Pigo kwa sekta ya michezo nchini Kenya Sportpesa ikisitisha ufadhili wake

-Kampuni ya kamare ya michezo, Sportpesa, imetamatisha ufadhili wake wa michezo yote ya humu nchini -Sportpesa ilichukuwa hatua hiyo baada ya serikali kuanza kutoza ushuru wa asilimia 35 kwa mapato yote ya bahati na sibu

-Kampuni ya kamare ya michezo, Sportpesa, imetamatisha ufadhili wake wa michezo yote ya humu nchini

-Sportpesa ilichukuwa hatua hiyo baada ya serikali kuanza kutoza ushuru wa asilimia 35 kwa mapato yote ya bahati na sibu

-Kampuni hiyo ilipinga ushuru kwa michezo ya bahati na sibu mahakamani na kupoteza kesi hiyo

Kampuni ya bahati na sibu kwenye michezo Sportpesa imetatatisha ufadhili wake wa michezo yote ya humu chini Kenya kuanzia Januari 1, 2017.

Sportpesa ilichukuwa hatua hiyo baada ya serikali kutangaza utekelezaji wa ushuru wa asilimia 35 kutoka kwa mapato yote ya bahati na sibu.

Sheria hiyo ilipendekezwa na waziri wa fedha Henry Rotich, akiweka ushuru wa asilimia 50 kwa michezo ya bahati na sibu aliposoma bajeti ya mwaka wa 2017/2018.

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhim pindi zinapochipuka

Habari Nyingine: Hakuna kusafiri usiku kuanzia leo na leseni zimefutwa - NTSA na polisi wafoka

Hata hivyo, pendekezo hilo lilipingwa vikali na kapuni za bahati na sibu zilizosema ushuru huo hauleti matunda yoyote.

Hatua hiyo iliisababisha Sportpesa kuwasilisha kesi katika mahakama kuu kupinga pendekezo hilo ambalo lilipitishwa na bunge la taifa.

Habari Nyingine: Familia ya Uhuru inawasaka kondoo wake 230,000 walioibwa kutoka Brookside dairy

Habari Nyingine: Wakili wa Uhuru amtafuta aliyekuwa mchezaji wa Arsenal, Emannuel Eboue

Hata hivyo, jaji wa mahakama kuu John Mativo alitupilia mbali kesi hiyo, akisema kuwa haki za mshitaki hazikukiukwa kama ilivyowasilishwa na kampuni za bahati na sibu.

Uamuzi huo uliisababisha Sportpesa kutamatisha ufadhili wake wa michezo yote ya humu nchini.

Habari Nyingine: Limousine ya KSh208 M iliyo na uwezo wa kwenda ardhini na majini (Picha)

Chama cha mchezo wa raga nchini (KRU) kimeshangazwa na uamuzi huo utakaokilazimisha kufanya mpango mwingine wa mchezo huo nchini ya mwaka wa 2018.

Sportpesa imechukuwa nafasi muhimu katika michezo nchini Kenya kwa kufadhili michezo na vilabu tofautoi vya michezo vya humu nchini, zikiwemo timu za soka za Gor Mahia na AFC Leopards.

Read ENGLISH VERSION

Una maoni? Una taarifa ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdia39xhZZmp6Kfn2K4uK2MrJykrJFixqJ5zKKaoZ2qpHqvr8eipaJlm5q7uq2MrKeoqqSlsrStjKKioquZqba0tMBmrJ%2BZlJ22rbWMsJiknV6dwa64

 Share!