- Mgogoro ulianza baada ya jamaa huyo kushindwa kusema zilipokuwa KSh 8,000 walizokuwa wamechanga kwa ajili ya mazishi ya mwenzao
- Marehemu ndiye aliyepewa jukumu la kuweka pesa za mchango huo ili kugharimia shughuli za msibani
- Jamaa waliokasirishwa na mwenzao walimpiga kitutu na hatimaye jamaa huyo kufariki akitibiwa katika Hospital ya Zimmerman
Wakaaji wa Zimmerman, Nairobi wanaomboleza kifo cha jamaa yao aliyepigwa kitutu na kuuawa na wenzake baada ya kudaiwa kula KSh 8,000 walizokuwa wamechanga kwa ajili ya mazishi ya mmoja wao aliyekuwa ameaga dunia.
Jamaa huyo alipigwa Jumamosi, Novemba 10 baada ya kukosa kusema zilipo pesa za mchango kwa ajili ya shughuli za msibani.
Habari Nyingine: Mtoto wa nyoka ni nyoka; bintiye Akothee ajianika nusu uchi
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/1120/0fgjhs6kteinsc04r.jpeg)
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Habari Nyingine: Mwanamke amshataki mpenziwe kwa kumuuma sehemu nyeti kitandani
Ripoti za NTV ambazo TUKO.co.ke ilizisoma zilisema kuwa, jamaa huyo ndiye aliyekuwa amepewa kazi ya kuhifadhi pesa za mchango na badala yake alizila.
Marehemu alipigwa hadi kupoteza fahamu, na kupelekwa Katika Kliniki ya Penda kupata huduma ya kwanza na hatimaye akaaga.
Habari Nyingine: Afisa wa trafiki acheza densi barabarani, asahau habari ya hongo (video)
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/720/0fgjhs7ut2fk32are.jpeg)
Habari Nyingine: Rais Uhuru akutana na mlinzi wake wa zamani mwaka mmoja baada ya kumpandisha cheo
Mwili wa marehemu ulipelekwa City Mortuary huku polisi nao wakiendelea na msako wa kuwatia mbaroni waliohusika na mauaji hayo.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdibn5zhJBmmKWhqZq4trjAZqeeq5Fix6J5zJqrmqaXlnqvrcirppuhXZa9qrPWmmSnmV2ssq%2FGwKScZqCRmbZut9SumLCZXp3Brrg%3D