- Etale alidaiwa kupokea milioni mbili ili kuiba mchujo huo
- Nduguye Ken Okoth alishinda kwa kuzoa kura zaidi ya alfu nne
-Etale amepuuzilia mbali madai hayo na kusema iwapo ni kweli atajiuzulu
Mwelekezi wa mawasiliano ndani ya chama cha ODM Philip Etale amesema atajiuzulu iwapo yeyote atatoa ushahidi kuwa alikula mlungula ili kuhakikisha Imran Okoth anashinda mchujo wa Kibra.
Etale amekerwa na ripoti kwenye mitandao kuwa alikabidhiwa mlungula wa shilingi milioni mbili ili amchezee Imran karata ndani ya chama hicho na kumfanya kuibuka mshindi.
Habari Nyingine: Maisha yangu yamo hatarini, mbunge Alice Wahome asema
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/1120/2cd37e9fdb814f81.jpeg)
Etale alijitetea kuwa hakujihusisha na siasa za Kibra kwa njia yayote wala kufanya mazungumzo yoyote na wagombea waliokuwa wakitafuta tiketi ya ODM.
Habari Nyingine: Ndindi Nyoro na Kamaina Kamanda wafanya kanisa kuchukua mkondo mpya
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/720/d0719cb53bdafe71.jpeg)
Imran alibwaga wagombea wengine 10 kwenye mbio za kutafuta tiketi ya chama hicho na sasa atakabiliana na wapinzani kutoka Jubilee na ANC.
Bendera ya Jubilee itapeperushwa na mwanasoka McDonald Mariga na ya ANC kubebwa na Eliud Owalo.
Uchaguzi huo mdogo ulisababishwa na kifo cha aliyekuwa mbunge Ken Okoth.
WanaKibra watapiga kura mnamo Novemba 7.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke; au WhatsApp: 07324826
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjZoF6fJBmp6GhnJ69brHTmqOeZZGptrS0yJpkpK2ansK7wcuuZJuZkZmubsXAZqKunJGexKJ5wKWgpK2clnquuNSnnq6kkWK2rbWMpKycoJWvrm63wKuYrZldoMSmutieZKabmKq3sHnKopmrmV6dwa64